Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 19

Kwa kuwa umekamilisha kipindi hiki, unaweza kutathmini jinsi umeweza kuyatimiza Malengo ya Somo la Kipindi hiki kwa kujibu maswali haya. Andika majibu katika Shajara yako na ujadiliane na Mkufunzi wako katika Mkutano saidizi wa Somo utakaofuata. Unaweza kulinganisha majibu yako na nakala kuhusu Maswali ya kujitathmini mwishoni mwa Moduli hii.

Swali la Kujitathmini 19.1 (linatathmini Malengo ya Somo 19.1 na 19.2)

Je, ni gani kati ya kauli hizi si sahihi? Eleza kisicho sahihi kwa kila kauli.

  • A.Kuta za misuli za mishipa ya damu za mwili wote wa mwanamke zinaponywea, nafasi ndani ya mishipa huongezeka na hivyo shinikizo lake la damu kushuka.
  • B.Hipatensheni katika ujauzito hupunguza damu inayotoka kwenye ateri za endometria kwenye uterasi ya mama hadi kwa fetasi kupitia kwa plasenta.
  • C.Hipatensheni hupunguza kiwango cha kiowevu cha amnioni kinaichozunguka fetasi kwa sababu kiasi cha damu inayoingia kwenye figo za mtoto ni kidogo na hivyo hutengeneza kiasi kidogo cha mkojo.
  • D.Ukuaji wa fetasi hauzuiliwi kwa mwanamke mjamzito aliye na hipatensheni.

Answer

A si kweli. Kuta za misuli za mishipa ya damu za mwili wote wa mwanamke zinaponywea, nafasi ndani ya mishipa hii hupungua, hivyo shinikizo lake la damu hupanda.

B ni kweli. Hipatensheni katika ujauzito hupunguza damu inayotoka kwenye ateri za endometria kwenye uterasi ya mama hadi kwa fetasi kupitia kwa plasenta.

C ni kweli. Hipatensheni hupunguza kiwango cha kiowevu cha amnioni kinaichozunguka fetasi kwa sababu kiasi cha damu inayoingia kwenye figo za mtoto ni kidogo na hivyo hutengeneza kiasi kidogo cha mkojo.

D si kweli. Kuna uwezekano mkubwa wa ukuaji wa fetasi kuzuiliwa kwa mwanamke mjamzito aliye na hipatensheni kwa sababu viwango vya oksijeni, virutubishi na viowevu vinavyomfikia mtoto kutoka kwa plasenta kupitia damu hupungua.

Mwisho wa jibu.

Swali la Kujitathmini 19.2 (linatathmini Malengo ya Somo 19.1 na 19.3)

Kamilisha Jedwali 19.3 kwa vipimo ambavyo ungetarajia kupata kwa wanawake walioainishwa kuwa na aina za hipatensheni zilizoonyeshwa katika upande wa mkono wa kushoto.

Jedwali 19.3 kwa Swali la Kujitathmini 19.2
AinaShinikizo la juu la damu ProtinuriaDalili za ukali
Hipatensheni ya ujauzito
Priklampsia ndogo
Priklampsia kali
Priklampsia zaidi juu ya iliyokuwepo awali

Answer

Jedwali 19.3 lililokamilishwa limeonyeshwa hapa chini.
AinaShinikizo la juu la damu ProtinuriaDalili za ukali
Hipatensheni yaujauzito (hutokea katika ujauzito na kuisha baadaye)zaidi ya kipimo cha 140/90 mmHgHakuna protinuria nyingiHakuna
Priklampsia ndogoKati ya 140/90 mmHg na 160/110 mmHgHakuna protinuria nyingiHakuna
Priklampsia kaliZaidi ya au sawa na 160/110 mmHgProtinuria inayoonekana iwepo au isiwepo (matokeo ya kipimo cha dipstick zaidi ya au sawa na +2)Maumivu ya kichwa, kiwaa, maumivu ya epigasriamu, kupungua kwa mkojo, kupungua au kutokuweko kwa kucheza kwa mtoto
Priklampsia zaidi juu ya iliyokuwepo awaliJuu kuliko kabla ya ujauzito kwa mwanamke aliye na hipatensheni suguProtinuria inayoonekana nyingi zaidi au inayozidi Kuwe au kusiwe na dalili za ukali

Mwisho wa jibu.

Soma uchunguzi maalumu ufuatao kisha ujibu maswali yatakayofuata.

Uchunguzi Maalum 19.1 Kisa cha Zewditu

Zewditu ni mwanamke primigravida mwenye umri wa miaka 37 na ana ujauzito wa pacha. Yeye ana uzani wa kupita kiasi ikilinganishwa na urefu wake. Mama huyu alikuwa mwenye afya njema hadi ujauzito wake ulipofika juma la 22, alipoanza kulalamikia maumivu ya kichwa na kuvimba nyayo na vifundo.

Swali la Kujitathmini 19.3 (linatathmini Malengo ya Somo 19.1, 19.2, 19.3, 19.4, 19.5 na 19.6)

  • a.Je, Zewditu ana visababishi vyovyote vya hatari vya hipatensheni vinavyotokea sana. Iwapo ndio, ni vipi?
  • b.Je, ana mojawapo ya dalili za kiafya za hipatensheni? Iwapo ndio, ni dalili na ni nini kisababishi?
  • c.Je, ni matatizo yapi yanayoweza kuathiri mtoto wa Zewditu iwapo hatatibiwa hipatensheni?
  • d.Je, ni hatua zipi utakazochukua katika kisa cha Zewditu, na ni kwa nini?

Answer

  • a.Zewditu ana visababishi vitatu hatari vya hipatensheni vinavyotokea sana: yeye anapata mtoto wake wa kwanza baada ya umri wa miaka 35; anatarajia pacha; na ni mnene kupindukia.
  • b.Ana dalili mbili za kiafya za hipatensheni: maumivu ya kichwa na kuvimba kwa nyayo/vifundo. Dalili hizi mbili husababishwa na edema (kuvimba kutokana na kiowevu kujikusanya kwenye tishu). Maumivu ya kichwa hutokana na edema kwenye ubongo, angali, kuvimba nyayo na vifundo hutokana na edema kwenye tishu za miguu. Kisababishi cha edema ni shinikizo la juu la damu linalosukuma kiowevu kutoka kwa damu kupitia kuta za mishipa kisha kuingia kwenye tishu zilizo karibu.
  • c.Matatizo yanayoweza kumuathiri mtoto wa Zewditu asipotibiwa haraka ni kuachia kwa plasenta, asifiksia ya ndani ya uterasi, kuzuiliwa kwa ukuaji ndani ya uterasi, fetasi kufia ndani ya uterasi au upunguani baadaye maishani.
  • d.Hatua ya kwanza ni kumpima shinikizo la damu na kuchunguza kuwepo kwa protini katika mkojo wake. Hata ikiwa matokeo ni karibu na kawaida, anapaswa kupewa rufaa hadi kituo cha ngazi ya juu zaidi, bila wewe kujaribu utatuzi wowote, ikiwezekana apewe rufaa hii siku hiyo ya uchunguzi. Hii ni kwa sababu hata ikiwa hipatensheni yake ni ndogo wakati huo, inaweza kuendelea na kuwa priklampsia kali kwa kipindi cha muda mfupi.

Mwisho wa jibu.

Muhtasari wa Kipindi cha 19