Malengo ya Somo la Kipindi cha 19

Baada ya kusoma somo hili, unapaswa uweze:

19.1 Kufafanua na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliochapishwa kwa herufi nzito. (Maswali ya Kujitathmini 19.1, 19.2 na 19.3)

19.2 Kueleza kwa kifupi kinachotendeka kwenye mishipa ya damu na viowevu vya mwili kwa wanawake walio na hipatensheni, na jinsi kinavyoweza kuidhuru fetasi. (Maswali ya Kujitathmini 19.1 na 19.2)

19.3 Kufafanua aina tofauti za magonjwa ya kihipatensheni ya ujauzito. (Maswali ya Kujitathmini 19.2 na 19.3)

19.4 Kuorodhesha visababishi vikuu vya hipatensheni inayohusiana na ujauzito. (Swali la Kujitathmini 19.3)

19.5 Kueleza dalili za kiafya zinazotokea sana za priklampsia kali. (Swali la Kujitathmini 19.3)

19.6 Kutambua matatizo yanayotokea sana ya magonjwa ya kihipatensheni ya ujauzito kwa mama na fetasi/mtoto mchanga. (Swali la Kujitathmini 19.3)

19.7 Kutoa matibabu saidizi ya kimsingi na kuwezesharufaa ya mapema, hasa kwa wanawake walio na magonjwa makali ya kihipatensheni ya ujauzito. (Swali la Kujitathmini 19.3)

Kipindi cha 19 Magonjwa ya Kihipatensheni ya Ujauzito

19.1 Je, hipatensheni huathiri vipi ujauzito?