19.1.1 Athari kwa mishipa ya damu na viowevu vya mwili

Tukio linalojulikana sana kwa mwanamke anayepata hipatensheni katika ujauzito ni kuwa kuta za misuli za mishipa ya damu mwilini mwote hunywea, na kwa hivyo nafasi ndani ya mishipa hupungua. (Jina maalum la hali hii ni msongo wa mishipa kote mwilini.) Msongo huu wa mishipa husababisha shinikizo la juu la damu katika mishipa ya damu, na hii ni sababu moja ya kiowevu kutoka kwa damu kusukumwa nje kupitia kuta za mishipa na kukusanyika kwenye tishu za mwanamke huyo.

  • Je, uvimbe unaotokana na kukusanyika kwa kiowevu kwenye tishu huitwaje, na ni wapi ambapo uvimbe unaoneka sana kwa wanawake wajawazito walio na hipatensheni? (Ulijifunza kuhusu haya katika Kipindi cha 7 na cha 8, hasa Kisanduku 8.2.)

  • Uvimbe huu huitwa edema na ni ishara ya hatari ya hipatensheni katika ujauzito. Huonekana mara nyingi katika sehemu ya chini ya miguu, vifundo na nyayo; pia mikono, na kwenye uso na mgongo katika hali kali sana.

    Mwisho wa jibu

19.1 Je, hipatensheni huathiri vipi ujauzito?

19.1.2 Athari za hipatensheni ya mama kwa fetasi