19.5 Dalili za kiafya za eklampsia

Ekilampsia hutokea mwanamke akikosa matibabu bora akiwa na priklampsia kali. Hili ndilo tatizo hatari sana la priklampsia kali. Inaweza kutokea kabla ya leba, katika leba na baada ya kuzaa. Wakati mwingine eklampsia inaweza kutokea kwa muda wa hadi saa 24 baada ya kuzaa, hata kwa wanawake waliozaa wakiwa na shinikizo la damu la kawaida na bila dalili zozote za hatari kabla na katika leba. Kwa hivyo mwanamke akija kwako na historia ya tukutiko baada ya leba na kuzaa kikawaida na hata wakati mwingine nyumbani, tatizo la kwanza la kiafya unalofaa kuzingatia ni eklampsia. Lakini unapaswa pia kujua kuwa kuna visababishi vingine vya tukutiko, kama vile kiwango cha chini au juu sana cha sukari katika damu (hipo au hipaglisimia), malaria yanayoathiri ubongo, maambukizi ya bakteria kwenye ubongo (kwa mfano meninjitisi), kiharusi, madawa, au kusumishwa.

Jinsi ulivyojifunza hapo juu, utambuzi wa eklampsia hufanywa dalili za kiafya za priklampsia zikiwepo, pamoja na:

  • Tukutiko
  • Koma bila ya visababishi vingine.

Tukutiko katika eklampsia huwa la ghafla mwanzoni lakini katika visa vingine huenda kukawa na ishara na dalili za hatari zinazothibitisha kutokea kwa eklampsia (tazama Kisanduku 19.2).

Kisanduku 19.2 Ishara na dalili za hatari zinazoonyesha kuwa eklampsia inatokea

  • Maumivu yasiyodhibitiwa kwa urahisi/makali ya kichwa
  • Maumivu makali ya epigastriamu
  • Kiwaa au kutoona kabisa (kwa muda)
  • Uchovu au kuwashwa
  • Kutotambua wakati (saa), watu, na mahali katika mazingira yake
  • Kutofahamu mazingira
  • Kuonyesha tabia zisizo za kawaida.

19.4.6 Edema ya mwili wote (ya patholojia)

19.5.1 Matukutiko katika eklampsia