19.6.2 Kuwashawishi wananwake walioathiriwa kwenda kwa matibabu ya kiafya

Unapaswa kutoa ushauri kwa mwanamke na familia yake kuhusu hatari ya matatizo ya mama na fetasi na umuhimu wa kupata matibabu ya kitaalamu mara moja. Katika visa vya eklampsia, watu katika sehemu nyingi za mashambani huamini kuwa matukutiko yanahusiana na roho za kishetani. Mwanamke mjamzito aliyepata tukutiko kwenye tamaduni hizi huenda asitake kwenda kituoni mwa afya kwa sababu angependelea kwenda kwa maji matakatifu, kasisi au kiongozi mwingine wa dini, au madaktari wa kienyenji. Una jukumu muhimu sana kuhakikisha kuwa mwanamke huyo na familia yake wameelewa kuwa matukutiko hayo husababishwa na shinikizo la juu la damu analopitia. Mhakikishie kuwa matukutiko hayo yatakoma baada ya kuzaa.

19.6.1 Hatua iwapo priklampsia si kali

19.6.3 .Matibabu saidizi ya priklampsia kali kabla ya rufaa