Muhtasari wa Kipindi cha 19

Katika Kipindi cha 19 umejifunza kuwa:

  1. Magonjwa ya hipatensheni katika ujauzito ndiyo mojawapo ya visababishi vinanavyotokea sana vya maradhi na vifo vya kina mama na vya wakati wa kuzaa.
  2. Msongo wa mishipa ya damu mwilini mwote ni tukio la hipatensheni inayohusiana na ujauzito. Hii huleta kupunguka kwa kiasi cha damu ya mwanamke, kwani viowevu hutoka kwenye mishipa ya damu na kujikusanya kwenye tishu. Edema hutokea kwenye tishu na ogani tofauti (zikiwemo ubongo, ini na figo) na kusababisha kupungua katika uletaji wa damu kwenye sehemu tofauti za mwili wa mama na kwenye plasenta.
  3. Visababishi vya hatari vinavyojulikana vya hipatensheni inayohusiana na ujauzito ni: kuwa primigravida kabla ya umri wa miaka 20 na baada ya miaka 35, ujauzito wa zaidi ya mtoto mmoja, historia ya kibinafsi au kifamilia ya priklampsia au eklampsia, kuwa na ugonjwa wa kisukari au figo au, unene wa kupindukia.
  4. Priklampsia (shinikizo la juu la damu + protini nyingi) ndiyo aina inayotokea sana ya hipatensheni katika ujauzito. Priklampsia kali huonyeshwa kwa dalili za kiafya kama vile maumivu ya kichwa, kiwaa, maumivu ya epigastriamu, kupungua kwa mkojo, kupungua kwa kucheza kwa mtoto na kuwa na edema ya mwili wote.
  5. Eklampsia hutambulika mwanmke mjamzito anapopata tukutiko au koma bila visababishi vingine. Ndicho kisababishi kikuu cha vifo vya kina mama na fetasi kati ya aina zote za magonjwa ya kihipatensheni ya ujauzito.
  6. Katika visa halisi, eklampsia ina awamu tatu: awamu ya utulivu, toni, kiklonasi na koma.
  7. Awamu ya koma inaweza kuwa ndefu iwapo kuna tukutiko la kujirudia, edema kubwa ubongoni, kutokwa na damu kwa wingi ndani ya kichwa, au hipoglisimia husika.
  8. Matatizo yanayotokea sana ya priklampsia kali ni eklampsia, anemia, kiwango cha chini cha pleteleti, kukosa kufanya kazi ghafla kwa ogani kadhaa (figo, ini, moyo, mapafu na macho).
  9. Matatizo ya fetasi ni kuachia kwa plasenta, asifiksia ya ndani ya uterasi, na asifiksia ya mapema ya mtoto mchanga (kutokana na kiwango cha chini cha oksijeni kwenye damu) uzuaji wa ukuaji kwenye uterasi na fetasi kufariki ndani ya uterasi.
  10. Katika udhibiti wa magonjwa ya kihipatensheni ya ujauzito, jukumu lako la kwanza ni kuwezesha rufaa mapema.

19.6.4 Rufaa ya dharura ya eklampsia

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 19