20.2.5 Njia za kutekeleza uavyaji mimba

Utoaji mimba wa kupanga uliosalama hutekelezwa kwa kina mama wanaofikia vigezo vya sheria vilivyoelezwa hapo juu na walio tayari kutamatisha ujauzito. Taratibu hutekelezwa kwa kituo cha afya au hospitali, kwa hivyo unapaswa kuwapa rufaa wanawake wanaotafuta huduma ya kutoa mimba wazuru kituo cha juu zaidi cha afya. Njia za kuendeleza utoaji mimba wa kisheria hutegemea umri wa kipindi cha ujauzito na vifaa vinavyopatikana mahali pale. Hujumulisha:

  • Tiba ya utoaji mimba: wanawake hupewa dawa za kutekeleza utoaji wa mimba
  • Aspiresheni ya tupu uliotengezwa kwa mkono: kutumia kifaa kama sindano kinachotumiwa kwa mkono na kusababisha shinikizo la hasi ili kufyonza nje na kuvuta viliyomo katika uterasi.
  • Uhamishaji na kuretaji: kutoa vitu vilivyomo katika uterasi kwa kutumia vifaa vya chuma kutoa tishu za fetasi na kusafisha kuta za ndani za uterasi.

Kumbuka kuwa wanawake huhitaji usaidizi wa kihisia kabla, baada na wakati wa kutoa mimba uliopangwa, kama vile wanavyohitaji baada ya mimba kutoka pekee yake. Katika kitengo kifuatacho, tutaeleza huduma unazopaswa kutekeleza kwa mwanamke baada ya kutoa mimba.

20.2.4 Mtazamo wa kisheria kuhusu utoaji mimba

20.3 Utunzaji wa mwanamke baada ya kutoa mimba