20.3.1 Malengo ya huduma baada ya kutoa mimba

Malengo ya utunzaji wa mwanamke baada ya kutoa mimba ni:

  • Kutoa huduma salama, zilizo na ubora wa hali ya juu.
  • Kupeleka huduma hadi kwa watu walio vijijini iwezekanavyo.
  • Iwe rahisi na inayokubalika kwa wanawake.
  • Kuelewa hali ya kipekee ya kijamii ya kila mwanamke na mahitaji yake binafsi, na kumpatia utunzaji wake ipasavyo.
  • Kupunguza idadi ya mimba zisizopangwa na utoaji wa mimba.
  • Kutambua na kuhudumia wanawake walio na mahitaji mengine ya kijinsia au mahitaji ya kiafya ya uzazi.
  • Iwe rahisi na inayodumu katika mfumo wa afya.

Ili kutimiza malengo haya, unao wajibu wa kutekeleza, pamoja na kutambua mahitaji ya kibinafsi na hali ya jamii ya wanawake binafsi na kuwaelekeza wanapoweza kupata utunzaji unofaa katika mahali panapofaa. Unapaswa pia kuchukua hatua inayofaa kuhusu barua yoyote ya rufaa ambayo mwanamke anaweza kurudisha kijijini kutoka kwenye kituo cha ngazi ya juu zaidi cha afya.

20.3 Utunzaji wa mwanamke baada ya kutoa mimba

20.3.2 Ujumbe muhimu kwa wanawake baada ya mimba kutoka pekee yake au uliopangwa