20.5.1 Wakati wa kuanza upangaji uzazi

Huduma ya upangaji uzazi baada ya kutoa mimba inapaswa kutekelezwa mara moja, kwa sababu uwezo wa kupata mimba hurudi haraka: katika wiki mbili baada ya kutoa mimba au kuharibika kwa mimba katika awamu ya kwanza, na utoaji wa mimba au kuharibika kwa mimba katika wiki ya nne baada ya awamu ya pili. Wanawake wote wanaopokea huduma baada ya kutoa mimba wanahitaji ushauri na habari kuhakikisha wataelewa kuwa wanaweza kupata mimba tena kabla ya awamu ya kwanza ya hedhi, na kwamba kuna mbinu salama za kuzuia mimba au kuchelewesha mimba.

Ikiwa mwanamke anataka kupata mimba tena hivi karibuni, mshawishi angoje. Miezi sita baada ya mimba kutoka pekee yake au kutoa mimba uliopangwa kuna uwezekano wa kuzaa mtoto aliye na uzito mdogo au mtoto kuzaliwa kabla ya muda wake na mama kupata anemia.

Katika kipindi kifuatacho, utaongezea kile umejifunza katika kipindi hiki tutakapoeleza sababu za kuvuja damu katika awamu ya mwisho ya ujauzito na namna ya kudhibiti hali hii ya dharura.

20.5 Upangaji uzazi baada kutoa mimba

Muhtasari wa Kipindi cha 20