Muhtasari wa Kipindi cha 20

Katika Kipindi cha 20, umejifunza kwamba:

  1. Kuvuja damu mapema wakati wa uajuzito hutokea kabla ya wiki 28 ya mimba.
  2. Utokaji wa mimba pekee yake (kuharibika kwa mimba) hutokea kwa takriban mimba 15%.
  3. Visababishi vya kawaida vya uvujaji wa damu mapema wakati wa ujauzito ni utoaji wa mimba uliopangwa au mimba kutoka pekee yake, mimba isiyokuwa katika sehemu yake, na isiyokuwa ya kawaida. Hali hizi zinaweza kusababisha matatizo makubwa, ikiwa ni pamoja na vifo vya wajawazito, hasa wakati mtu asiyekuwa na ujuzi atatoa mimba kwa njia isiyo kuwa salama katika mazingira ma machafu.
  4. Ruhusa ikitolewa, wanawake wanaweza kupata huduma za utoaji wa mimba uliosalama katika vituo vya afya. Matibabu na Upasuaji zipo zakuuchagua huduma ya kutoa mimba kwa njia iliyosalama ukizingatia sheria.
  5. Dalili hatari baada ya kutoa mimba ni pamoja na uchungu mkali wa spazimu katika sehemu ya chini ya fumbatio, fumbatio uliovimba au ulio mgumu, kuvuja damu nyingi, harufu mbaya kutoka ukeni, joto jingi mwilini, mdundo wa haraka katika mshipa, kichefuchefu, kizunguzungu na mshtuko. Hizi ni dalili kwamba matibabu ya dharura na rufaa zinapaswa kuanza mara moja.
  6. Matibabu ya dharura ya kuvuja damu au mshtuko ni pamoja na kutilia dawa kwa mshipa kabla ya kumpeleka mama kwenye kituo cha afya, akiandamana na mtu anayeweza kumpatia damu.
  7. Upangaji uzazi inapaswa kuwa nzuri kwa mwanamke baada ya huduma ya kutoa mimba, ili kuvunja anuai katika hali ya utoaji wa mimba uliopangwa na kumpatia muda wa kupata nafuu katika hali ambazo mimba ilitoka pekee yake.

20.5.1 Wakati wa kuanza upangaji uzazi

Maswali ya kujitathmini ya kipindi cha 20