21.1 Kuvuja damu katika awamu za mwisho wa ujauzito husababishwa na nini?

Kuvuja damu katika awamu za mwisho za ujauzito au kuvuja damu kabla ya kuzaa mara nyingi husababishwa na kuvuja damu kutoka kwa plasenta, ingawa kuna visababishi vingine vichache vinavyotokea katika uterasi au sehemu zingine za mfumo wa uzazi. Kwanza, tutaorodhesha visababishi hivi kwa ufupi, kisha kufasili kwa kina kuhusu plasenta kujitenga kutoka pembezoni mwa uterasi, privia ya plasenta na kupasuka kwa uterasi, kwa sababu hizi ni hali zinazohitaji huduma ya dharura ili kuokoa maisha.

  • Kutengeka kwa plasenta: hali hii hutokea iwapo plasenta itatengeka kabla ya wakati (mapema sana) kutoka kwenye sehemu yake ilipojibandika kwa kawaida katika thuluthi mbili juu ya uterasi.
  • Privia ya plasenta: hali hii hutokea wakati plasenta imejibandika katika sehemu ya chini sana ya uterasi, ikikaribia seviksi sana, au hata kuifunika.
  • Kupasuka kwa uterasi: hali hii inaweza kutokea iwapo leba itadumu kwa muda mrefu au leba itazuiliwa, ambapo uterasi huraruka au kupasuka baada ya majaribio mengi ya kusukuma fetasi.
  • Kupasuka kwa vena ya varikosi katika eneo la uke: hii hutokea iwapo vena imejipinda na kupanuka. Hivyo basi, uterasi inaweza kujeruhiwa kwa urahisi na kuvuja, hasa katika leba na kuzaa.
  • Utetelezi mkuu: ute uliochanganyika na damu unaotoka ukeni kuashiria mwanzo wa leba huitwa utetelezi; wakati mwingine, kizibo hiki cha ute kinapotoka kinaweza kufuatiwa na uvujaji mkubwa wa damu unaoitwa utetelezi mkuu, ambao hukoma peke yake bila usaidizi wowote. Hata hivyo, mama anapaswa kupendekezewa rufaa kila wakati.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 21

21.2 Kutengeka kwa plasenta: