21.2.1 Mshtuko unaohusiana na kuvuja damu

Hali zote zinazotokea kufuatia kutengeka kwa plasenta zinakuhitaji uchukue hatua ya dharura: tazama Kitengo 21.5.

Tukio la kutengeka kwa plasenta linaloambatana na kuvuja damu nje au ndani ya uterasi linaweza kusababisha mshtuko unaohusiana na kuvuja damu, ambapo damu huvuja kwa kiasi kikubwa hivi kwamba damu inayosalia katika mishipa ya mwanamke haitoshi kufikisha virutubishi na oksijeni inayohitajika kwenye seli zake.

  • Dalili za mshtuko unaohusiana na kuvuja damu ni zipi? (Rejelea Kisanduku cha 20.3 katika kipindi cha awali)

  • Mwanamke mwenye mshtuko ataparara na kulowa jasho huku akiwa na mrindimo hafifu lakini wa kasi (zaidi ya midundo 100 kwa dakika), kupumua kwa haraka, shinikizo la chini la damu au linaloshuka (shinikizo la kidiastoli — kiwango cha chini — halizidi 60 mmHg na wakati mwingine ni la chini sana); anasema ana kizunguzungu; anaonekana kuchanganyikiwa na hata kupoteza fahamu.

    Mwisho wa jibu

Unapaswa kutambua dalili kama vile kuparara: kucha, viganja vya mikono na sehemu ya ndani ya kigubiko cha macho huendelea kuwa nyeupe pindi anavyoendelea kupoteza damu. Mwanamke huyu anaweza kukwambia kuwa anachoka au kushindwa kuinua kichwa chake. Yeye pia huonekana kutotulia, pengine anaomba kunywa maji, na anaonekana kuchanganyikiwa. Kuchanganyikiwa hutokea kwa sababu ubongo haupati oksijeni ya kutosha. Madhara ya mshtuko yanayotokea mara nyingi kufuatia kuvuja damu ni pamoja na figo au moyo kushindwa kufanya kazi.

21.2 Kutengeka kwa plasenta:

21.2.2 Hali kali ya kushindwa kwa figo