21.4 Uterasi iliyopasuka

Kuvuja damu kufuatia kupasuka uterasi kunaweza kutokea kupitia ukeni, hivyo unaweza kuona damu ikitiririka nje, au uterasi inaweza kuvujia damu ndani ya fumbatio ambapo haitaweza kuonekana. Ikiwa mwanamke mwenye leba iliyodumu kwa muda mrefu ataanza kuhisi maumivu katika fumbatio, (mauvimu yanayoendelea na kuzidishwa na mwendo wowote), au uterasi ikikoma kukazana katika jaribio la kumsukuma mtoto, au damu kuanza kuvuja ukeni ikiandamana na mshtuko, kuna uwezekano kuwa uterasi imepasuka. Ikiwa uterasi itakoma kukazana, fumbatio litakuwa laini na utaweza kuzihisi sehemu za mwili wa mtoto kwa urahisi kwa kulichunguza fumbatio. Ikiwa mtoto amekufa, hutaweza kusikia mpigo wa moyo wake hata kwa fitoskopu.

Utajifunza kwa kina kuhusu hali ya kupasuka uterasi katika Moduli inayofuata katika mtaala huu, kuhusu Utunzaji katika Leba na Kuzaa. Unapomhudumia mwanamke mwenye dalili za kupasuka uterasi, unafaa kuchukua hatua za dharura kama inavyoelezwa hapa chini.

21.3 Privia ya plasenta

21.5 Jinsi ya kushughulikia mwanamke anayevuja damu katika awamu za mwisho za ujauzito