Muhtasari wa Kipindi cha 21

Katika kipindi cha 21, umejifunza kwamba:

  1. Kuvuja damu katika awamu za mwisho wa ujauzito kunaweza kusababisha kifo cha mama na fetasi, hivyo hali hii inapaswa kuchukuliwa kama jambo la dharura linaloweza kuhatarisha maisha.
  2. Visababishi vya mara nyingi vya tukio la kuhatarisha maisha la kuvuja damu katika awamu za mwisho wa ujauzito ni kutengeka kwa plasenta kabla ya wakati, na privia ya plasenta, au kwa nadra sana linaweza kutokea kufuatia kupasuka uterasi.
  3. Hali isiyo kali sana ya kuvuja damu inaweza kutokea kufuatia vena ya varikosi ukeni, au damu kutokana na utetelezi mkuu, ambao husita bila usaidizi wowote.
  4. Kutengeka kwa plasenta kabla ya wakati kunaweza kutokea kama hali fiche ya kuvuja damu (kuvujia ndani) au hali wazi (damu inaonekana kwa nje) kutoka ukeni; damu hii kwa kawaida huwa na uweusi na mwanamke anaweza kuwa na maumivu ya fumbatio.
  5. Privia ya plasenta mara nyingi hudhihirika kama damu yenye wekundu mng’avu na isiyosababisha maumivu, na inaweza kuhusishwa na utangulizi mbaya ya fetasi. Kwa kawaida, (lakini sio kila mara) fetasi huwa katika hali ya kawaida.
  6. Usimchunguze uke wa mwanamke anayevuja damu katika awamu za mwisho wa ujauzito kwa sababu unaweza kuzidisha kuvuja damu.
  7. Hatua za kwanza muhimu katika kudhibiti mshtuko unaohusiana na kuvuja damu katika wanawake wanaovuja damu sana katika awamu za mwisho za ujauzito ni kufanya ukadiriaji wa mwanzoni wa ishara muhimu na kuanzisha matibabu ya kutia viowevu mishipani.
  8. Baada ya kumtia viowevu mishipani, mhamishe mwanamke huyu haraka hadi katika Hospitali ya Wilaya au kituo cha afya kilicho na chumba cha upasuaji, kwa sababu visa vingi huhitaji upasuaji.

21.5 Jinsi ya kushughulikia mwanamke anayevuja damu katika awamu za mwisho za ujauzito

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 21