Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 21

Kwa sababu umekamilisha somo hili, unaweza kutathmini ulivyofanikisha Malengo yake kwa kujibu maswali yafuatayo. Andika majibu yako katika shajara kisha ujadiliane na Mkufunzi wako katika mkutano utakaofuata wa Somo saidizi. Unaweza kulinganisha majibu yako na vidokezo kuhusu Maswali ya Kujitathmini yaliyo mwishoni mwa moduli hii.

Swali la Kujitathmini 21.1 (linatathmini Malengo ya Somo 21.2 na 21.3)

Jamaa wa mwanamke mmoja wamekuita kumhudumia mwanamke anayevujia damu ukeni katika miezi 8 ya ujauzito.

  • a.Utafanya nini katika uchunguzi wako wa kwanza?
  • b.Utamwanzishia matibabu ya dharura na kumpendekeza rufaa aende katika kituo cha afya kilicho karibu? Eleza ni kwa nini ndivyo au sivyo.
  • c.Utaawaambia jamaa zake wafanye nini?

Answer

  • a.Uchunguzi wa kwanza utakuwa kutathmini haraka hali zote za mwanamke, pamoja na ishara kuu: mdundo wa moyo, shinikizo la damu, pumzi na halijoto; mchunguze kama ana hali ya kuparara, uchovu, kizunguzungu, au kuchanganyikiwa.
  • b.Matibabu ya dharura yanapaswa kuanzishwa haraka iwezekanavyo kwa kumtia mishipani kiowevu cha Chumvi ya Kawaida au mchanganyiko wa Laktesi ya Ringer. Hatua hii itaokoa maisha yake kwa kuongeza chumvi na viowevu vilivyopotezwa kufuatia kuvuja damu, hivyo shinikizo lake la damu halitashuka sana hadi kiwango cha hatari.
  • c.Jamaa zake wanapaswa kufahamishwa watayarishe chombo cha kumsafirisha mwanamke hadi katika kituo kikuu cha afya kilicho karibu.

Mwisho wa jibu

Maswali ya Kujitathmini 21.2 (linatathmini Malengo ya Somo la 21.1, 21.2 na 21.3)

Ni maelezo yapi yafuatayo yasiyo ya kweli? Katika kila kauli, eleza lisilo la kweli.

  • A.Unaweza kumchunguza uke wa mwanamke mjamzito aliyekuja kwako akivujia damu ukeni katika wiki ya 37 ya ujauzito.
  • B.Kutengeka kwa plasenta kabla ya wakati wake kwa kawaida husababisha kuvuja damu inayotokea ukeni.
  • C.Privia ya plasenta hutokea iwapo plasenta imejibandika karibu na seviksi au kuifunika.
  • D.Ikiwa damu itakoma kuvuja bila usaidizi wowote, unaweza kutompendekezea rufaa mwanamke anayevuja damu sana katika awamu za mwisho za ujauzito, au ana kuvuja kunakorejea.

Answer

A si kweli. Haupaswi kamwe kumchunguza uke wa mwanamke anayevuja damu katika awamu za mwisho wa ujauzito.

B si kweli. B Kutengeka kwa plasenta kutoka mahali pake pa kawaida kabla ya wakati kunaweza kusababisha damu kuvujia nje, lakini pia kunaweza kusababisha damu kuvujia ndani.

C ni kweli. Privia ya plasenta hutokea wakati plasenta imejibandika katika sehemu inayokaribia seviksi au kuifunika.

D sio kweli. D Unapaswa kila wakati kumpendekezea rufaa mwanamke anayevuja damu kwa muda mrefu katika awamu za mwisho za ujauzito hata ikiwa damu itakoma kuvuja bila usaidizi wowote.

Mwisho wa jibu

Soma Kauli ya Somo 21.1 kisha ujibu maswali yanayofuata.

Unchunguzi Maalum 21.1 Bi. X ameletwa katika Kituo cha Afya

Bi X ameletwa katika Kituo chako cha Afya akiwa amebebwa na jamaa zake huku amelazwa kwenye kitanda cha mbao cha kujitengenezea nyumbani. Unafahamishwa kuwa ana ujauzito wa miezi 9. Alianza kwa kuumwa na fumbatio kisha kuvuja damu ukeni. Unapomchunguza, unatambua kuwa nguo zake zimelowa damu. Ana wasi wasi na kiu. Mapigo yake ya moyo ni midundo 120 kwa dakika, na shinikizo la damu ni 80/50 mmHg.

Swali la Kujitathmini 21.3 (linatathmini Malengo ya Somo 21.1 na 21.2)

  • a.Ni visababishi vipi vinavyoweza kupelekea kisa hiki? Fafanua jibu lako.
  • b.Je Bi X yoko katika hali ya mshtuko? Thibitisha utambuzi wako.

Answer

  • a.Visababishi vinavyoweza kupelekea kisa cha Bi X ni:
    • Kutengeka kwa plasenta
    • Privia ya plasenta
    • Uterasi iliyopasuka
    • Kupasuka kwa vena ya varikosi.
  • b.Bi X yuko katika hali ya mshtuko: yeye hatulii na ana kiu, mrindimo wake ni wa kasi mno (midundo 120 kwa dakika) na shinikizo lake la damu liko chini sana hata kumhatarishia maisha (80/50 mmHg).

Mwisho wa jibu

Muhtasari wa Kipindi cha 21