Malengo ya Somo la Kipindi cha 22

22.1 Kufasili na kutumia kwa usahihi maneno yote muhimu yaliyoandikwa kwa herufi nzito (Maswali ya kujitathmini 22.1, 22.2 na 22.3)

22.2 Kueleza sababu za kumpa mwanamke mjamzito matibabu ya kumdungia viowevu mishipani au kumwingiza katheta ndani ya kibofu (Swali la Kujitathmini 22.1 na 22.3)

22.3 Kufafanua kuhusu vifaa utakavyotumia, maandalizi na utaratibu wa kuanzisha matibabu ya kudungia viowevu mishipani pamoja na jinsi ya kuchagua sehemu bora ya kutoboa mshipa wa vena, kuweka na kutoa kanula kwenye mishipa. (Maswali ya Kujitathmini 22.1 na 22.2)

22.4 Kufafanua jinsi ya kufuatilia matibabu haya. (Swali la Kujitathmini 22.1)

22.5 Kufafanua kuhusu vifaa utakavyotumia, maandalizi na mbinu ya kuingiza na kutoa katheta ya mkojo. (Maswali ya Kujitathmini 22.1 na 22.3)

22.6 Kufafanua kuhusu taratibu za kudhibiti maambukizi zinazohitajika ili kupunguza hatari ya kupata maambukizi yanayotokea kufuatia mbinu ya kudungia viowevu mishipani na kutia katheta kwenye kibofu. (Swali la Kujitathmini 22.1 na 22.2)

Kipindi cha 22 Kuanzisha Matibabu ya Kudungia Viowevu Mishipani na Kumwingiza Katheta Mwanamke Mjamzito

22.1  Kuanzisha matibabu ya kudungia viowevu mishipani