22.1  Kuanzisha matibabu ya kudungia viowevu mishipani

22.1.2 Wakati bora wa kuanzisha matibabu ya kudungia viowevu mishipani

Mwanamke mjamzito anayevuja damu atapata hali ya mshtuko kwa haraka sana; anaweza kupoteza fahamu na kisha kufa iwapo hautafanya lolote kwa haraka.

  • Je, dalili za mshtuko ni zipi? (Ulijifunza haya katika Kipindi cha 20.)

  • Mwanamke atapata uweupe hasa ndani ya vigubiko vya chini vya macho na viganja vya mikono yake; shinikizo lake la damu la kidiastoli (la kipimo cha chini) likiwa chini ya 60 mmHg- na wakati mwingine likiwa chini zaidi na mpigo wa moyo ukiwa juu; mara nyingi ukiwa zaidi ya midundo 100 kwa kila dakika.

    Mwisho wa jibu

Ili kuokoa maisha yake, unapaswa kufahamu jinsi ya kuanzisha matibabu ya kudungia viowevu mshipani (ambayo pia hujulikana kama ufufuzi wa kutumia viowevu vinavyodungiwa mishipani au kutia viowevu mishipani).

Hii inamaanisha kuingiza viowevu maalum ndani ya mzunguko wa damu kwa kutumia sindano iliyo na shimo inayoitwa kanula. Sindano hii huingizwa mishipani ili kutia viowevu vitakavyochukua nafasi ya sehemu ya viowevu vya damu vinavyopotezwa. Unapaswa kuyafanya haya kabla ya kumhamisha kwa dharura hadi kituo cha afya atakapopewa damu. Wanawake walio katika leba au muda tu baada ya kuzaa wanaweza kuvuja damu (kama utakavyojifunza katika Moduli ya Utunzaji katika Leba na Kuzaa). Unafaa kuanzisha matibabu ya kudungia viowevu mishipani kwa haraka utakapogundua kuwa mwanamke anavuja damu.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 22

22.1.2 Kutayarisha vifaa vya matibabu ya kudungia viowevu mshipani