22.1.5 Kuchagua sehemu ya kudungia

Mchoro 22.2 Sehemu za kudunga mshipa kwenye mkono na kigasha.

Hatua inayofuatia ni kutambua sehemu bora ya kudunga mshipa wa vena, yaani sehemu ambapo ‘utatoboa mshipa’ kwa kuingizia kanula ya kutilia viowevu. Mchoro wa 22.2 unaonyesha sehemu za kawaida zinazotumika kwenye mkono na kigasha.

Ili kuchagua eneo la kudunga mshipa wa vena:

  • Mwulize mgonjwa akuonyeshe mkono anaotumia mara nyingi, kwa mfano, kushikia kisu au chombo chochote kile. Ikiwa atasema ni 'mkono wa kulia', huu ndio mkono 'ulio na nguvu zaidi' na mkono wake wa kushoto 'hauna nguvu sana'.
  • Kwanza, tafuta sehemu utakazodunga kwenye mkono wake usio na nguvu ukizingatia sehemu ya juu katika mkono huu.
  • Chagua mshipa unaotoshea kanula huku ukiepuka maeneo yalio karibu na viungo kama vile kifundo au kiwiko.
  • Hakikisha kuwa baada ya kumwingiza mwanamke huyu kanula, kanula hii haitatizi uwezo wake wa kusongesha mkono.
  • Epuka eneo lililo na maumivu likiguswa

Uwezakano wa mshipa kuonekana unaweza kuimarishwa kwa kumhimiza mwanamke akunje na kukunjua vidole vyake mara kadhaa na kupeleka mkono wake chini huku ukisugua eneo la kudunga.Unapoendelea kupata ujuzi, itakuwa rahisi kwako kuchagua mshipa mwafaka unaoonekana vyema, ambao haujajipinda kisha mahali unafikiri unaweza kuingiza kanula yako kwa urahisi.

22.1.4 Kuchagua kanula ya sindano

22.1.6 Kuingiza kanula ya kutia viowevu mishipani