22.4  Kuingiza katheta ndani ya kibofu

Mwanamke mjamzito aliye kwenye leba asiyeweza kukojoa kufuatia kufinyika kwa mrija wa kupisha mkojo (urethra) kutoka kwenye kibofu atasumbuka sana. Vile vile, kibofu kilichojaa kitazuia mtoto kuzaliwa kwa kuchukua nafasi kwenye pelvisi. Kwa, anahitaji katheta (mpira safi au neli ya plastiki) iingizwe ndani ya kibofu ili kuupisha mkojo kabla hujampa rufaa aende kwenye kituo cha afya cha kiwango cha juu. Mbinu hii huitwa uwekaji katheta. Utaratibu wa kuweka katheta unaweza kuruhusu uzalishaji kuendelea. Mwanamke hataweza kuzaa kwa njia ya kawaida bila utaratibu huu iwapo leba itaanza. Wanawake wanaokuwa na leba ya muda mrefu, pia wanaweza kuhitaji kuwekewa katheta ikiwa vibofu vyao vimezuiliwa. Kibofu cha mwanamke kilichovimba huhisi kama mfuko laini wa maji uliojitandaza juu ya mfupa wa kinena. Unaweza kuona kibofu chote kama mwinuko wenye umbo la duara akilala chali.

Mfahamishe utakachomfanyia na umueleze umuhimu wa utaratibu huo. Baadaye mwambie alale chali huku kichwa kikiinuliwa na kuikunja na kupanua miguu. Funika upande wa chini wa mwili wake kwa kitambaa safi isipokuwa eneo la ukeni ili asiaibike iwapo kuna watu wengine karibu.

22.3.2 Wakati unaofaa wa kusitisha kuingiza viowevu mshipani

22.4.1 Vifaa vya kuingizia katheta ndani ya kibofu