Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 22

Kwa kuwa umekamilisha kipindi hiki, unaweza kutathmini jinsi ulivyofanikisha Malengo ya Somo hili kwa kujibu maswali yanayofuatia. Andika majibu yako kwenye Shajara yako ya Masomo na uyajadili na Mkufunzi wako katika Kikao Saidizi kitakachofuata. Unaweza kulinganisha majibu yako na Muhtasari katika Maswali ya Kujitathmini yaliyo mwishoni mwa Moduli hii.

Swali la Kujitathmini la 22.1 (linatathmini Malengo ya Somo 22.1, 22.2, 22.3, 22.4, 22.5 na 22.6)

Ni maelezo yapi kati ya yafuatayo ambayo si kweli? Katika kila kauli, eleza lisilo la kweli.

  • A.Mwanamke aliye katika hali ya mshtuko kufuatia kuvuja damu nyingi anafaa kupewa rufaa haraka bila kuanzishiwa matibabu ya kudungia viowevu mishipani.
  • B.Ikiwa eneo lililodungwa litafura na kuwa chungu, ondoa kanula kisha uiweke mahali pengine.
  • C.Ikiwa hauna plasta ya kubandikia juu ya sehemu iliyodungwa, hakuna haja ya kudhibiti kanula mshipani.
  • D.Ikiwa shinikizo la damu na mpigo wa moyo wa mwanamke umerejea hali ya kawaida na havuji damu tena, unaweza kusitisha viowevu.
  • E.Sirinji hutumika kuingiza maji safi kwenye kifuko cha kukusanyia mkojo unaotoka kwenye kibofu na kupitia kwenye mrija.
  • F.Nawa mikono yako kabisa kwa sabuni na maji kabla ya kumgusa mgonjwa au kifaa chochote.
  • G.Kima cha mtiririko kinafaa kuwa cha haraka iwezekanavyo unapoanzisha matibabu ya kudungia viowevu mshipani mwa mwanamke aliye katika hali ya mshtuko.

Answer

A si kweli. Mwanamke aliye katika hali ya mshtuko (shinikizo la chini la damu na mpigo wa haraka wa moyo) kutokana na kupoteza damu huhitaji kuanzishiwa matibabu ya kudungia viowevu mishipani kabla ya kupewa rufaa.

B ni kweli. Ikiwa eneo lililodungwa limefura na ni chungu, unafaa kuondoa kanula na kuidungia mahali pengine. Hii inaonyesha kuwa viowevu vinaingia ndani ya tishu badala ya mshipa.

C si kweli. Ikiwa huna plasta ya kubandikia juu ya eneo lililodungwa, unapaswa kudhibiti kanula kwa kuifunga kwa nguo safi. Kanula inaweza kutoka nje ya mshipa ikiwa haitadhibitiwa.

D ni kweli. Ikiwa shinikizo la damu na mpigo wa moyo wa mwanamke umerejea hali ya kawaida na havuji damu tena unaweza kusitisha viowevu.

E si kweli. Sirinji ni ya kuingizia maji safi kwenye puto la katheta (si kwenye kifuko cha kukusanyia mkojo) ili kufurisha puto na kufanya katheta isalie ndani ya kibofu.

F ni kweli. Kabla hujamgusa mgonjwa au kifaa chochote, unafaa kunawa mikono kabisa kwa sabuni na maji.

G ni kweli. Kima cha mtiririko katika mwanamke aliye katika hali ya mshtuko kinafaa kuwa cha haraka iwezekanavyo punde tu unapomwanzishia matibabu ya kudungia viowevu mishipani wake.

Mwisho wa jibu

Swali la Kujitathmini 22.2 (linatathmini Malengo ya Somo 22.1, 22.3 na 22.6)

Panga upya orodha ifuatayo katika utaratibu sahihi wa hatua unazofaa kuchukua unapoanza matibabu ya kudungia viowevu mishipani.

Using the following two lists, match each numbered item with the correct letter.

  1. Nawa mikono yako.

  2. Mlaze mgonjwa

  3. Vaa glavu safi.

  4. Tambua sehemu unayoweza kuingizia kanula.

  5. Fungilia fundo la kuzuia damu hadi takriban upana wa vidole vitatu juu ya eneo hili.

  6. Safisha eneo utakalodunga ukitumia antiseptiki, alkoholi au sabuni na maji.

  7. Chukua kanula kutoka kwenye kifurushi safi kisha uiingize mishipani katika sehemu uliyochagua, kisha uondoe sindano huku ukiiacha kanula ya plastiki mishipani.

  8. Fungua kifurushi cha mrija safi kisha ukiunganishe na kifuko cha viowevu, halafu ukininginize juu ya mgonjwa au umwagize mtu yeyote akishikilie juu yake.

  9. Unganisha kanula na kifuko kilicho na viowevu kisha ufungue klampu ya duara.

  • a.5.

  • b.9.

  • c.8.

  • d.3.

  • e.1.

  • f.2.

  • g.7.

  • h.6.

  • i.4.

The correct answers are:
  • 1 = e
  • 2 = f
  • 3 = d
  • 4 = i
  • 5 = a
  • 6 = h
  • 7 = g
  • 8 = c
  • 9 = b

Swali la kujitathmini 22.3 (linatathmini Malengo ya Somo 22.1, 22.2 na 22.5)

Fasili kuingiza katheta na umuhimu wake kwa mwanamke mjamzito aliye katika leba. Orodhesha angalau vifaa vitano unavyohitaji ili kufanya utaratibu huu.

Answer

Kuingiza katheta ndani ya kibofu ni kutia mpira safi au mrija wa plastiki ndani ya kibofu kupitia kwenye urethra ili kuondoa mkojo wakati kibofu kimezuiwa. Kibofu kinaweza kuzuiliwa katika leba inayodumu kwa muda mrefu ama leba iliyozuiliwa mtoto akifinya urethra na kufunga mtiririko wa kawaida wa mkojo.

Vifaa unavyohitaji ni:

  • Katheta safi yenye ukubwa sahihi (FK16)
  • Mrija safi wa kufyonza na kifuko cha kukusanyia mkojo
  • Sirinji iliyo na maji safi ya kufurisha puto ya katheta
  • Glavu safi
  • Alkoholi au mchanganyiko wa antiseptiki na pamba.
  • Mrija wa mafuta ya kulainisha
  • Mwangaza
  • Nguo ya kumfunika mwanamke sehemu ya chini ya mwili

Mwisho wa jibu

Muhtasari wa Kipindi cha 22